Pongezi hizo zimetolewa na Waheshimwa Madiwani wakati wa Baraza la kujadili Bajeti ya mwaka 2026-2027 lilifanyika leo tarehe 3 Februari 2026 katika ukumbi katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya korogwe uliyopo Makuyuni.
Katika Baraza hilo lililoudhuriwa na Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mhe.Wiliam Mwakilema,Afisa Tarafa ya Mombo Ndg. Alex Mhando,Wataalamu wa Halmsahauri,TARURA,RUWASA na Wageni mbalimbali.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe Mhe.Selemani Mwongozo Aliwapitisha Washeshimiwa Madiwani katika bajeti hiyo kisha kuridhia kupitisha bajeti hiyo.
Sambamba na kupitisha Bajeti hiyo Mhe.Mwongozo alikaribisha maswali ya papo kwa papo kutoka kwa Wakala wa barabara za Vijijini (TARURA) na Mamlaka ya Maji RUWASA ambapo Waheshimiwa Madiwani waliuliza maswali mbalimbali na kutoa maoni juu ya huduma zinazotolewa na taasisi hizo.
Aidha Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Mwakilema alipata nafasi ya kuzungumza ambapo alitoa maelekezo juu ya Mpango wa suala la Bima ya Afya kwa wote ambapo utagharimu shilingi 150,000 kwa watu sita ikilenga kuwanufaisha Wananchi wote kwa ujumla.Pia Mkuu wa Wilaya ya Korogwe alisisitiza suala la kutunza mazingira katika vyanzo vya maji ili kundokana Na upungufu wa Maji unaowakabili Wananchi kwa sasa.Vile vile Mhe. Mwakilema alisisitiza suala la kulinda usalama ambapo kila Raia anajukumu la kulinda usalama wa Nchi.



Korogwe District Council
Postal Address: P.o Box 584
Telephone: 027- 2650017/2650061
Mobile:
Email: ded@korogwedc.go.tz
Haki miliki©2016 KDC Haki zote zimehifadhiwa